Search

Translate

MAANA YA TIBA NINI KATIKA MAISHA YA MWANADAMU?

TIBA

Tiba (au: Uganga) ni elimu kuhusu magonjwa ya binadamu mwilini na rohoni, jinsi ya kuzuia magonjwa na kurudisha uzima. Matibabu ni muhimu kwa afya ya binadamu na yanahitajika sana ili kumpa maisha mazuri.

Tiba imeendelea kiasi cha kuwa na matawi yanayoangalia hasa:

magonjwa ya sehemu fulani tu ya mwili, kwa mfano tiba ya moyo, ya ngozi, ya viungo vya ndani, au

aina ya tiba, kwa mfano upasuaji, au

aina ya watu, kwa mfano magonjwa ya watoto na kadhalika.

Kila somo dogo lina wataalamu wake.

Watu wanaoshughulikia magonjwa ya watu huitwa matabibu au waganga. Mara nyingi watu huwaita "daktari", lakini neno hili lamaanisha zaidi cheo cha kufaulu chuo kikuu kwenye ngazi ya juu; mara nyingi waganga husoma hadi cheo cha daktari wa tiba.

Watu wanaofanya kazi pamoja na tabibu ni muuguzi (nesi) na wasaidizi wengine.

Elimu hiyo inayofuata mbinu za kisayansi ni tofauti na uganga wa kienyeji au wa kimila.

TIBA KATIKA MAGONJWA

Ugonjwa au maradhi ni hali ya mvurugo katika utendaji wa kawaida wa shughuli za mwili na roho inayoathiri vibaya ustawi au starehe ya kiumbehai. Hivyo hakuna tofauti kamili baina ya ugonjwa na hali ya kujisikia vibaya.

Sayansi inayochungulia magonjwa ni sayansi ya tiba.

Magonjwa yanaweza kugawanyika kutokana na vyanzo/asili zake kama vile:

magonjwa ya kuambukiza

magonjwa ya kurithi

magonjwa kutokana na ajali

magonjwa kutokana na dutu za nje ya mwili (sumu, asidi) au moto

magonjwa ya kansa

magonjwa yaliyosababishwa na tiba

magonjwa yaliyosababishwa na mfumo wa kingamaradhi uliomo mwilini

magonjwa ya nafsi

magonjwa ya roho








0 Reviews:

Contact Form

Name

Email *

Message *