Search

Translate

Je! Ni faida gani za usimamizi wa wakati

 

KUNAFAIDAGANI YA MUDA KATIKA MAISHA YA VIUMBE?

Maisha
Jump to navigationJump to search
Maisha ni muda ambao kiumbe hai anajaliwa kuishi. Ni hali tofauti kabisa na uzima wa milele, kwa kuwa uhai wake una mwanzo na mwisho.

Hasa mwisho unasababisha maswali: kama kila chenye mwanzo kina mwisho, ya nini kuwepo kwake? Kukosa lengo, kuwepo bure, kutokuwa na maana kunamfanya mtu ajisikie mnyonge, pengine akate tamaa ya kuishi, la sivyo ajitose kufurahia mazuri yanayopatikana maishani, lakini bila uwezo wa kuondoa moyoni ule utupu wa maana unaomtia huzuni ya dhati.

Ndiyo sababu maana ya maisha ni mojawapo kati ya masuala makuu ya binadamu duniani: hawezi kukwepa maswali ya kutoka moyoni mwake kuhusu thamani, madhumuni na umuhimu wa maisha yake.

Suala hilo linaweza kujitokeza kwake katika maswali mengi tofauti yanayohusiana, kama vile: "mbona tumekuwepo?"; "maisha yanahusu nini?" na "nini maana ya hayo yote? Binadamu anajiuliza maswali kama hayo hasa anapokabiliana na kifo, kwa mfano msiba wa ndugu au rafiki.

Hilo limekuwa suala kuu la udadisi wa sayansi, falsafa na dini tangu zamani. Hivyo kumekuwa na idadi kubwa ya majibu kutoka asili mbalimbali kadiri ya itikadi na utamaduni

SIKU NINI?
Siku ni muda wa saa 24 ambamo tunaona vipindi viwili: kile cha mwanga wa mchana na kile cha giza la usiku.

Mchana na usiku
Mabadiliko hayo ya mchana na usiku husabibishwa na mzunguko wa dunia kwenye mhimili wake. Upande wa dunia unaotazama jua unapata mwanga wa mchana lakini upande mwingine usiotazama jua unakuwa gizani.

Sisi pamoja na vitu vyote vilivyo juu ya uso wa dunia, yaani bahari, mito, milima, binadamu, misitu, majangwa, majengo, barabara na kila kitu unachoweza kuwaza kuwa kipo kwenye uso wa dunia, basi vyote huwa katika mwendo kadiri dunia inavyojizungusha kwenye mhimili wake. Hivyo basi, wakati upande ule wa uso wa dunia tulipo unapogeukia au kutazamana na jua, basi kwetu inakuwa mchana, pale ambapo upande huo hatutazamani na dunia, basi tunapata usiku, yaani tunakuwa kwenye giza.

Mwanzo na mwisho
Mwanzo na mwisho wa siku ni jambo la mapatano baina ya watu ma hapa kuna kawaida tofautitofauti katika tamaduni za Dunia.

Uchumi na sheria siku hizi hufuata muda sanifu wa dunia unaopanga mwisho na mwanzo wa siku ya kalenda katikati ya usiku, yaani saa sita usiku, au kwa lugha nyingine kwenye 24:00 au 0:00 h.

Kalenda za kidini kama kalenda ya Kiyahudi na Kalenda ya kiislamu hupanga mwisho wa siku wakati wa machweo, ambayo ni pia mwanzo wa siku mpya. Kwa sababu hiyo sherehe ya Sabato katika Uyahudi (ambayo inalingana na Jumamosi ya Kiswahili) inaanza baada ya machweo kwenye Ijumaa, na pia utaratibu wa kuzuia kazi unakwisha kwenye jioni ya Jumamosi baada ya machweo.

Muda wa siku
Mzunguko huo wa dunia kwenye mhimili wake unachukua muda wa nukta (sekunde) 86,400 au masaa 24.

Kwa sababu muda wa mzunguko haulingani kikamilifu na kipimo cha sekunde kuna siku ndefu au fupi zinazopatikana kwa kuingiza au kupunguza nukta moja kufuatana na azimio ya wataalamu wa wakati. Hii haina umuhimu wowote katika maisha ya kila siku lakini inapaswa kuangaliwa pale ambapo saa kamili sana ya kiatomi hutumiwa.

Siku na mwaka
Dunia, pamoja na kujizungusha kwenye mhimili wake, ina mwendo mwingine pia , yaani ule wa kulizunguka jua. Ikikamilisha mwendo huu basi mwaka unakuwa umekamilika. Kipindi cha mwaka hakilingani kwa kila mwaka: kuna miaka mirefu na miaka mifupi. Hii ni kwa mujibu wa Kalenda ya Gregori ambapo mwaka wa kawaida (mfupi) huwa na siku 365 na kila mwaka wa nne (mwaka mrefu) kuwa na siku 366

MCHANA 

Mchana ni kipindi chote cha siku ambapo nuru ya jua inaangaza sehemu fulani ya dunia.
Kinyume chake ni usiku.
Kwa wakati mmoja, jua linaangaza karibu nusu ya dunia. Huko ni mchana, kumbe katika nusu ya pili ni usiku.
Kwa binadamu na wanyama wengi ndio wakati wa utendaji mwingi zaidi.

Nuru (kutoka Kiarabu نور, nur; pia mwanga) ni neno la kutaja mnururisho unaoweza kutambuliwa kwa macho yetu. Kwa lugha ya fizikia ni sehemu ya mawimbi ya sumakuumeme yanayoweza kutambuliwa na jicho.

Mawimbi ya nuru huwa na masafa ya nanomita 380 hadi 780 au yenye marudio ya takriban terahezi 789 hadi 384.

Chanzo cha nuru duniani ni hasa jua. Nuru ya jua inaleta pia nishati inayotumiwa na mimea ambayo kwa njia ya usanisinuru inajenga kwa ndani sukari au wanga ambavyo ni lishe za viumbehai vyote vinavyozila. Hivyo nuru ya jua, kwa njia ya usanisinuru, ni chanzo cha nishati kwa karibu viumbehai vyote duniani.

Chanzo kingine cha nuru kwa binadamu ni moto. Lakini hadi karne ya 19 nuru hii ilitumia pia nishati ya jua iliyotunzwa na mimea kwa njia ya kuni, mafuta ya petroliamu au gesi asilia. Ni tangu kugunduliwa kwa umeme tu ya kwamba chanzo tofauti cha nuru kimepatikana.

Nuru inayoonekana kwetu ni sehemu ya mnururisho wa sumakuumeme. Nuru inayoonekana ni sehemu ndogo tu ya spektra ya sumakuumeme.
Wanyama wanaweza kuona mawimbi marefu zaidi, yaani infraredi, au mafupi zaidi, yaani urujuanimno.

Aina nyingine za mnururisho huohuo ni kwa mfano joto, eksirei, microwave, mawimbi ya redio ambazo zinatofautiana na nuru kwa idadi ya marudio yake na hazitambuliwi kwa macho au milango ya fahamu, isipokuwa joto linalotambuliwa na ngozi yetu.

Tabia za nuru
Kati ya tabia za nuru zinazoweza kutofautishwa ni ukali wake, mwelekeo wake, marudio yake.
Kasi ya nuru haibadiliki: ni daima mita 299,792,458 kwa nukta katika ombwe.
Rangi ya nuru inategemea marudio yake.

MAANA YA USIKU NINI?
Usiku ni kipindi cha siku kilichopo kati ya machweo na macheo na hasahasa kipindi cha giza kinachotokea baada ya machweo ambapo mwanga wa jua hauonekani tena angani hadi muda mfupi kabla ya macheo yaani kabla ya jua kuonekana juu ya upeo wa anga.

Kinyume chake ni mchana.

Kutokana na kupoteapotea kwa nuru ya jua, nyota zinaonekana usiku (pasipo mawingu).

Watu wengi pamoja na wanyama wengi hulala usiku, lakini kuna wanyama wengine wanaofanya shughuli zao usiku kama vile bundi, popo na wadudu wengi.

Nyakati za usiku
Nyakati za mwanzo na mwisho wa usiku hutofautiana kati ya mahali na mahali duniani. Mstari unaofikiwa na mwanga wa jua unatembea juu ya uso wa dunia kutokana na mzunguko wa dunia kwenye mhimili wake.

Mwendo huu ndio sababu ya kugawiwa kwa uso wa dunia katika kanda muda.

Karibu na ikweta muda wa usiku ni masaa 12 sawa na muda wa mchana, lakini penginepo duniani, kadiri palipo mbali na ikweta kuelekea kaskazini au kusini, muda wa usiku hubadilika kila siku.

Usiku mrefu kabisa hutokea kwenye ncha za dunia ambako wala jua wala utusitusi havionekani angani kwa muda wa karibu miezi 3.

Utamaduni
Katika tamaduni za binadamu usiku mara nyingi una maana mbaya kutokana na matatizo ya kutoona vema na hofu ya vitu visivyoonekana katika kipindi hicho.

1.MUDA

Muda ni sisawasawa  na siku katika masiku ya siku 7

2.Msaa ni hesabu zinazo tajwa kwa kumaanisha uwepo wa naangapi katika masaa 12 yasiku na masaa ya usiku 12 ambayo ni sawa na masaa 24

Muda ni kipindi ambacho mtu aidha alifanya, anafanya au anatarajia kufanya jambo fulani. Katika maisha tumepitia vitu mbalimbali, baadhi tunaweza tukavikumbuka na vingine hatuvikumbuki, na katika maisha kadri muda unavyokwenda ndivyo vitu vinazidi kugunduliwa kutokana na ongezeko la sayansi.


Katika maisha ya kila siku mwanadamu hutegemea sana muda ili kufanikisha malengo yake.

Matumizi ya muda

Muda hutumika na watu mbalimbali kwa mambo mbalimbali kama itakavyoelezwa hapa chini:

mwanafunzi hutumia muda wake hasa kwa ajili ya kujisomea.

mfanyakazi hutumia muda wake hasa kwa ajili ya kujiendeleza kimaisha.

Endapo watautumia muda huo vibaya, hakika hawataweza kufikia malengo waliyojiwekea.


Hata hivyo ni muhimu kuwa na uwiano mzuri katika matumizi ya muda, kwa mfano, kwa sala na kazi.

MASAA

Saa ni kipimo cha wakati. Si kipimo cha SI kamili kama ilivyo sekunde lakini ni kawaida kote duniani pia katika matumizi ya kisayansi.

Saa inagawiwa kwa dakika 60 na sekundi 3,600. Siku ina takriban masaa 24.

Wakati ni neno la kutaja ama ufuatano wa matokeo au muda ama kipindi ambamo jambo latokea.

Tunaishi katika wakati na tunapanga maisha yetu kufuatana na wakati lakini si rahisi kusema wakati ni kitu gani. Sayansi, fizikia, falsafa na dini zote zina njia mbalimbali za kuangalia na kueleza wakati

Wakati kama mpito

Katika maarifa ya kila siku wakati ni utaratibu wa mfululizo wa matokeo. Tunaweza kuona ya kwamba jambo liliwahi kutokea (wakati uliopita), linaendelea sasa (wakati wa kisasa) na tunatarajia litaendelea katika wakati ujao. Hivyo ndivyo tunatazama maisha yetu tukikumbuka mambo yaliyopita, tunasikia hali au mambo yanayoendelea na kutegemea kuona siku inayokuja.

Kwa sababu hiyo kuna usemi kama "wakati unapita" au "wakati unakimbia".

Wakati kisayansi

Sayansi hutumia wakati kwa vipimo vingi hata kama haijui wakati mwenyewe ni kitu gani. Imeunda vipimo vya wakati mwenyewe vinavyowezesha kuelewa matokeo na kuyalinganisha.

Hapa sayansi inajaribu kuona wakati kama wanda (dimensioni) moja ya ulimwengu pamoja na zile tatu za nafasi ya ulimwengu. Hapa huitwa "wanda ya nne" (the fourth dimension).

Tofauti yake na nyanda za nafasi ni ya kwamba wakati una mwendo na mwelekeo.

Vipimo vya kawaida vya wakati

Vipimo vya wakati hutumia matokeo yanayorudia mara kwa mara bila mabadiliko.

Kipimo cha kawaida ni siku au kwa lugha nyingine muda wa mzunguko 1 wa dunia yetu unaonekana kwetu kutokana mabadiliko ya mchana na usiku.

Muda huu wa Mzunguko mmoja hugawiwa kwa masaa 24 na kuitwa "siku". Saa hugawiwa kwa dakika 60 na kila dakika kwa sekunde 60.

Mbio mmoja wa dunia yetu kuzunguka jua huitwa "mwaka". Utaratibu wa miaka hupangwa kwa njia ya kalenda.

Vipindi kama mwezi na wiki hupanga siku ndani ya kalenda.


Vipimo vya Kisayansi

Sayansi haijaridhika tena na vipimo hivi vya kawaida. Mizunguko ya dunia au siku hazilingani kikamilifu. Hapa sayansi imeondoka katika siku kama msingi wa vipimo vya wakati. Badala yake imechukua muda wa sekunde na kukiliganisha kwa mwendo wa atomi.

Katika vipimo sanifu vya kimataifa sekunde imewekwa kama muda wa radidi (periodi) 9,192,631,770 za mnururisho wa atomi ya caesi ya 133Cs.

Kisayansi Saa dio chombo maalum hutumka kupima wakati hasa saa za kronogilafia (chronograph watches) - saa zijulikanazo kwa Kingereza kama "Stop-Watch" za kupimia mda mfupi wakati tukio kama shindano la riadha zinafanyika


Vipindi vya wakati

milenia = miaka 1000

karne = miaka 100

mwaka = miezi 12 = siku 365.25

mwezi ≈ wiki 4 ≈ siku 30

wiki (juma)= siku 7

siku = masaa 24

saa = dakika 60

dakika = 60 sekunde

sekunde = 1000 millisekunde

milisekunde = 1000 mikrosekunde

mikrosekunde = 1000 nanosekunde

nanosekunde= 1000 pikosekunde

pikosekunde= 1/1,000,000,000,000 sekunde

1.MWAKA  2028

Mwaka ni kipindi cha takriban siku 365 katika Kalenda ya Gregori ambayo imekuwa kalenda ya kawaida kimataifa ikifuata mwendo wa jua.

Mwaka katika kalenda ya jua

Katika kalenda za jua mwaka unalingana na muda wa mzunguko mmoja wa dunia kwenye mzingo wake kuzunguka jua letu.

Muda kamili wa mzunguko huu ni siku 365.2425.

Kwa sababu hiyo kalenda ya Gregori inaongeza mwaka mrefu wa siku 366 katika utaratibu ufuatao:

kila mwaka wa nne utakuwa na siku 366 badala ya 365 kwa kuongeza tarehe 29 Februari. Mifano: 1892, 1996, 2004, 2008, 2012

kila mwaka ambao namba yake inagawiwa kwa 100 utakuwa na siku 365 (siyo 366 hata kama namba za miaka hii zinagawiwa kwa 4 pia!). Mifano: 1700, 1800, 1900, 2100

kila mwaka ambao namba yake inagawiwa kwa 400 utakuwa tena na siku 366 (siyo 365 hata kama namba za miaka hii zinagawiwa kwa 100 pia!). Mifano: 1600, 2000, 2400, 2800

Miaka katika kalenda mbalimbali

Katika kalenda mbalimbali kuna mahesabu tofauti ya muda wa mwaka.

Mwaka wa Kiislamu ni mwaka wa mwezi una siku 354.

Mwaka wa Kiyahudi unafuata pia kalenda ya mwezi lakini kwa namna ya pekee ya kuupatanisha na mwendo wa jua; muda wake ni siku 354 lakini kila baada ya miaka miwili au mitatu kuna mwaka mrefu kwa kuongeza mwezi mmoja. Kwa jumla mwezi huingizwa mara 7 katika kipindi cha miaka 19.

Kalenda za kihistoria ya Wamaya katika Amerika ya Kati ilikuwa na aina ya mwaka mwenye kipindi cha siku 260 iliyounganishwa na mwaka wa jua wa siku 365 katika utaratibu wa miaka 52.

Kalenda ya mwaka wa Kanisa ni kalenda inayoratibu sikuu za kikristo na utaratibu wa liturgia kama vile masomo ya Biblia kwa ajili ibada mbalimbali. Hii ni lazima kwa sababu namna ya kuratibu mwaka si miezi bali wiki na jumapili. Kalenda hii hutofautiana kiasi kati ya makanisa yenye mapokeo ya kiorthodoksi upande mmoja na kanisa katoliki upande mwingine. Waorthodoksi huhesabu kwenye msingi wa kalenda ya Juliasi na Wakatoliki huhesabu kwenye msingi wa kalenda ya Gregori. Makanisa ya kiprotestant kama vile Anglikana na Walutheri hufúata mapokeo ya kikatoliki. Tofauti si muda wa mwaka lakini mwanzo wake. Mwaka wa Kanisa huanza kewenye jumapili ya kwanza ya majilio au Adventi

2.MWEZI  NA TAREHE

Mwezi ni mojawapo wa vipindi kumi na mbili vya mwaka. Muda wa mwezi unategemea aina ya kalenda inayotumika

Uso wa mwezi jinsi unavyoonekana duniani hubadilikabadilika. Mwezi mpevu unaonekana kama duara kamili la kung'aa lakini baada ya kuonekana hivi umbo lapungua kila siku hadi kutoonekana kabisa na hali hii huitwa mwezi mwandamo. Baadaye mwezi unaonekana tena kama hilali nyembamba na kuongezeka hadi kuwa duara tena. Muda wa mabadiliko yote kupita mara 1 ni siku 29 1/4.

Muda wa mabadiliko kati ya mwezi mwandamo hadi kupotea na kuwa mwezi mwandamo tena ni kati ya siku 28 - 29. Kipindi hiki kinakumbukwa kirahisi, kinatazamiwa na watu wote wakati uleule kwa hiyo pamoja na kipindi cha siku kilikuwa kati ya vipimo vya kwanza vya wakati kwa binadamu.

Inawezekana kwamba juma la siku saba lilianza kwa kuzingatia robo 4 za mwezi wa siku 28.

Awamu za mwezi zilikuwa vipindi vya kuhesabu wakati tangu mwanzo wa kalenda. Hadi leo kuna kalenda ya mwezi ndiyo kalenda ya Kiislamu inayopanga wakati kutokana na hali halisi ya awamu za mwezi.

1,Januari , siku 31

2,Februari , siku 28

3,Machi , siku 31

4,Aprili , siku 30

5,Mei , siku 31

6,Juni , siku 30

7,Julai , siku 31,

8,Agosti , siku 31

9,Septemba , siku 30

10,Oktoba , siku 31

11,Novemba , siku 30

12,Desemba , siku 31

kwa kiarabu

Muharram محرّم

Safar صفر

Rabi`-ul-Awwal (Rabi' I) ربيع الأول

Rabi`-ul-Akhir (Rabi' II) ربيع الآخر أو ربيع الثاني

Jumaada-ul-Awwal (Jumaada I) جمادى الأول

Jumaada-ul-Akhir (Jumaada II) (Jumaada II) جمادى الآخر أو جمادى الثاني

Rajab رجب

Shaaaban شعبان

Ramadan رمضان

Shawwal شوّال

Dhul Qaadah ذو القعدة

Dhul Hijjah ذو الحج

4.SIKU KATIKA SIKU 7 YANI

Juma (kutoka neno la Kiarabu) au wiki (kutoka Kiingereza "week") ni kipindi cha siku saba. Kila siku ina jina lake.

Katika mwaka wa kalenda ya Gregori mna majuma 52 pamoja na siku moja au mbili za ziada. Hesabu ya majuma inaendelea mfululizo bila ya kuanza upya wakati wa mwaka mpya.

Ufuatano wa majuma haulingani na mgawanyo mwingine wa wakati kwa njia ya miezi au mwaka.

Mapokeo ya Kiyahudi-Kikristo

Asili ya juma ni katika utamaduni wa kale wa Mashariki ya Kati tangu Babiloni. Imeenea duniani kote kupitia Biblia na desturi za Uyahudi na Ukristo.

Ufuatano wa siku katika mapokeo hayo huanza na Jumapili. Majina ya siku ni kama yafuatayo:

Jumapili (Dominika)

Jumatatu

Jumanne

Jumatano

Alhamisi

Ijumaa

Jumamosi (Sabato)

Katika mwaka juma moja la Machi mwishoni au la Aprili linaadhimishwa na Wakristo wengi kama Juma kuu, ambapo wanaadhimisha matukio makuu ya imani yao kadiri ya historia ya wokovu, yaani mateso, kifo na ufufuko wa Yesu Kristo.

Siku za Jumamosi na Jumapili mara nyingi huitwa "wikendi" (kutoka Kiingereza: "weekend", yaani mwisho wa juma). Hata hivyo katika mapokeo hayo Jumapili ni mwanzo wa wiki mpya, si mwisho wake.

Majina ya siku kwa Kiswahili

Majina ya siku tano kwa Kiswahili ni ya namba zinazoanza kuhesabiwa baada ya siku ya Ijumaa (ambayo ni siku ya sala kuu katika Uislamu): Ijumaa - Jumamosi - Jumapili - Jumatatu - Jumanne - Jumatano.

Alhamisi na Ijumaa ni majina ya lugha ya Kiarabu inayofuata mapokeo ya Kiyahudi kuhusu majina ya siku.

Hivyo "Alhamisi" ina maana ya "siku ya tano" (baada ya Jumamosi inayoitwa "sabat" kwa Kiarabu, sawa kama "shabbat" kwa Kiebrania (lugha ya Wayahudi).

"Ijumaa" ni matamshi ya Kiswahili ya jina la Kiarabu la "jum'a" inayomaanisha "siku ya mkutano" (= ya kusali pamoja)

ILI KUJUWA FAIDA ZA MASAA NA MAANA YAKE 

unapaswa kujuwa kila saa ina kuwa na maana yake katika kila jambo utakalo taka kulifanya hapa kwenye linki hii utajuwa masaa pamoja na kila kinacho husika katika saa ikiwa unahitaji kufanya chochote katika shugulizako unatakiwa kupanga muda nakujifunza kufanya mambo yako kwamuda 


bonyeza hapa kupata 👉{YANAYO HUSU KILA SAA KATIKA MASAA 12}👈






0 Reviews:

Contact Form

Name

Email *

Message *